HAKUNA DHEHEBU LA DINI AMBALO LIKO JUU YA LINGINE, MADHEHEBU YOTE YAKO SAWA KISHERIA - RAIS SAMIA


"Hakuna Dhehebu Ambalo liko Juu ya Dhehebu lingine, Madhehebu Yote yako sawa Kisheria" ๐Ÿ‘‰Kauli hii imekuja wakati ambapo

TEC imekuwa ikitoa matamko yenye Mwelekeo wa kukosoa au kutoa tahadhari juu ya mwenendo wa kisiasa, kiuchumi, au kijamii.

Serikali inapitia kipindi cha mjadala mkubwa kuhusu uhuru wa maoni, siasa za ushindani, na mahusiano kati ya serikali na taasisi za dini. Kumekuwepo maneno ya mgawanyiko mitandaoni kuhusu utendaji wa serikali ya awamu ya sita.

Rais anajibu mijadala hii kwa kujaribu kurejesha mjadala katika misingi ya utulivu, umoja ambayo imekuwa kaulimbiu yake mara kwa mara.

Tutazame Ujumbe kwa taasisi za dini๐Ÿ‘‰

Rais Samia ameeleza wazi kuwa Matamko ya TEC yamekuwa mengi na yenye mgawanyiko ndani yao Anasema ndani ya Kanisa lenyewe kuna wanaopingana kuhusu matamko hayo.

Hii inaashiria kwamba serikali inaona baadhi ya matamko hayo hayawakilishi wote, hivyo kupunguza uzito wake wa kisiasa.

Anatoa onyo dhidi ya kutumia dini kama chombo cha mgogoro Hili ni jambo nyeti sana katika nchi yoyote.

Ametaja wazi kwamba “hakuna eneo baya la kumpata mtu kama dini”, akimaanisha nguvu ya dini inaweza kuwa chanzo cha kugawa jamii na kuanzisha migogoro ya hatari.

Anataka taasisi za dini zizingatie nafasi yao ya kufanya maadili, amani na mshikamano, badala ya kuingia kwenye malumbano ya kisiasa.

๐Ÿ‘‰Ujumbe kwa wananchi na wapinzani Rais ametumia hoja kadhaa za msingi๐Ÿ‘‡

Utawala wa demokrasia “Kama humpendi Samia, tustahimili tu... Ataongoza ataondoka.”

Serikali yake haipaswi kuangaliwa kama ya kudumu, bali kama inayofuata utaratibu wa kidemokrasia, hivyo hakuna sababu ya vurugu.

๐Ÿ‘‰Kukosoa kunaruhusiwa lakini si vurugu Amesema watu wana haki ya kukosoa “kama amefanya makosa, semeni makosa yake.”

Huu ni ujumbe kwamba ukosoaji si tatizo, tatizo ni ukosoaji unaopelekea kuchochea mgawanyiko au vurugu. Kutotumia chuki ya kikabila, kidini au kibinafsi

Rais Aligusia suala la kumchukia kiongozi
๐Ÿ‘‰Kwa asili yake
๐Ÿ‘‰Kwa dini yake
๐Ÿ‘‰Kwa alikotoka
๐Ÿ‘‰Au kwa sababu za mitazamo binafsi

Hii inalenga kuzuia siasa za chuki ambazo Afrika zimeleta migogoro mikubwa.

Ujumbe kuhusu mafanikio ya serikali Rais ametaja “makosa” kwa mtindo wa balagha
๐Ÿ‘‰Kuongeza huduma bora za afya
๐Ÿ‘‰Kuboresha elimu hadi vijijini
๐Ÿ‘‰Kukuza uchumi
๐Ÿ‘‰Kuimarisha usalama

Serikali yake inaonekana kukosolewa kwa mambo ambayo kwake ni mafanikio, hivyo ukosoaji huo umejengwa kwenye hisia, si hoja.

Nihitimishe Uchambuzi huu kwa kusema 
๐Ÿ‘‡
Ujumbe huu una uzito kwa sababu Unalenga kuweka mstari kati ya dini na siasa, ili kuepusha mgawanyiko wa kijamii. Kukemea propaganda zinazolenga kuleta taharuki nchini.

Ni hotuba nzito kisiasa, kiusomi, na ki-uhusiano kati ya serikali na taasisi za dini, yenye lengo la kuongoza mjadala wa umma kuelekea utulivu na siasa za hoja, si chuki.

Mwenyezi Mungu Ibariki Tanzania, Mwenyezi Mungu Ibariki Africa na Viongozi wake Wote (Ameen)

Baki na Mimi kwa Mengi zaidi yanayo jiri Duniani 

By Professor Chotara Mweusi Sultan kutoka viunga vya ๐Ÿ‘‡ 
๐Ÿ‘‰Sharif shamba 
๐Ÿ‘‰Ilala Dar es salaam 
๐Ÿ‘‰Tanzania 

Bingwa la uchambuzi wa maswala ya kijamii, Uchumi na Siasa za Dunia Yetu.


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

WALIOCHUKUA FOMU CCM ZA KUWANIA USPIKA HAWA HAPA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

๐Œ๐‰๐”๐„ ๐Š๐€๐‚๐‡๐„๐‘๐Ž ๐Œ๐™๐„๐๐€

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI