Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Morogoro, Beatrice Njawa ameviahidi vikundi vitano vya Wajasiriamali kuvipeleka kushiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam 2027, endapo vitafanya vizuri katika mafunzo ya siku tatu ya ujasiriamali ya "Jifunze kwa Mama Ujasiriamali" yaliyoandaliwa na Jukwaa Huru la Wahariri Tanzania (JUWATA) kwa ushirikiano na Taasisi ya Mamo Enterpreurship kwenye Ukumbi wa Bwalo la JKT Umwema mjini Morogoro kuanzia Julai 13 hadi 15, 2026.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Morogoro, Beatrice Njawa (katikati), akisindikizwa na Mwenyekiti wa JUWATA, Richard Mwaikenda (kushoto) na Katibu Mkuu wa Jukwaa hilo, Ahmad Mohamed baada ya kufungua mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na zaidi ya wananchi 800.

Comments