WANAFUNZI 50 KUPELEKWA UGHAIBUNI KUSOMA FANI YA AKILI UNDE

Serikali imetangaza wanafunzi 1,050 waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka 2026 watakaonufaika na mpango wa Samia Scholarship.

Kati yao, wanafunzi 50 bora zaidi watapelekwa kusoma nje ya nchi katika fani za Akili Unde (Artificial Intelligence - AI), Data Science na teknolojia nyingine za kisasa, huku wanafunzi 1,000 wakipata ufadhili wa kusoma katika vyuo vikuu vya ndani.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema mpango huo unalenga kukuza vipaji vya wanafunzi wa masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati (STEM) ili kuandaa wataalamu watakaosaidia maendeleo ya Taifa.

Amesema uteuzi umezingatia alama halisi za mitihani na wanafunzi waliopatikana wametoka katika tahasusi mbalimbali za sayansi zikiwemo PCM, PCB, PMG na PMC.

Serikali itagharamia masomo ya wanafunzi hao kwa asilimia 100, huku majina ya waliochaguliwa yakipatikana kupitia tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

Soma Taarifa ya UTEUZI:Rais Jakaya Kikwete amemteua Dkt. Ben E. Moshi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya PUMA Energy (zamani ilijulikana kama BP Ltd)

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

MAAFISA JENERALI WASTAAFU 17 WA JWTZ WAAGWA.

PICHA YA RAIS ILIYOBAMBA WIKI HII

18 WAPITISHWA KUGOMBEA UONGOZI YANGA

JUA AINA NNE ZA KABILA LA WASUKUMA

BINTI WA KITANZANIA GLORIA MAJULE ASHINDA TUZO YA UANDISHI BORA WA FILAMU YA MALARIA MAREKANI ‎

DK MAGUFULI ATANGAZA KIAMA CHA MAJAMBAZI, WEZI NA MAFISADI KATIKA MIKUTANO YA KAMPENI SUMBAWANGA,TUNDUMA, ILEJE NA MBOZI

ZIJUE SIFA ZA WANYAKYUSA WA KYELA NA RUNGWE