GAMOND: PACOME YUPO TAYARI KUANZA KUCHEZA


 KOCHA Mkuu wa Yanga, Miguel Gamondi ameibuka na kusema kiungo wake, Pacome Zouzoua yupo tayari kuanza kucheza na leo Jumatano kuna uwezekano akampa nafasi, lakini itategemea na mazoezi ya mwisho.

.

Mara ya mwisho Pacome kuonekana uwanjani akiitumikia Yanga ilikuwa Machi 17, mwaka huu walipofungwa mabao 2-1 na Azam katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa Uwanja wa Mkapa, na siku hiyo aliumia na kutolewa uwanjani.

.

Akizungumzia utayari wa Pacome kucheza mechi ya dhidi ya Tabora United, Gamondi amesema: “Anaweza kuwepo kwa sababu hivi sasa ameanza kufanya mazoezi ya kawaida, tutaangalia katika mazoezi nini kitatokea lakini inawezekana akacheza.”

.

“Kama tusingekuwa na mechi hii (dhidi ya Tabora United), basi uhakika mechi ijayo ya ligi (Mei 5 dhidi ya Mashujaa) angeanza kucheza angalau kwa dakika 30.”


Nene Yanga Fans HQ

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

YANGA BADO POINTI 2 TU ITANGAZE UBINGWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

CHATANDA ANENA MAKUBWA MAADHIMISHO SIKU YA FAMILIA DUNIANI

PROF NDAKIDEMI: TULETEENI MIRADI, TUWALIPE NYAMA NA SAMAKI

DKT NCHIMBI AZURU KABURI LA JOHN KOMBA LITUHI, NYASA