WANANCHI MKOA WA ARUSHA WAANZA RASMI KUNEEMEKA NA KLINIKI YA KUSIKILIZWA

Na Mwandishi wetu, Arusha


Vilio, nyuso za Huzuni, Majonzi na sura zilizokufa Matumaini ni mambo yaliyotawala kwenye Nyuso za mamia ya Wakazi wa Mkoa wa Arusha waliojitokeza kwa wingi kwenye Kliniki Maalum ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Paul Christian Makonda ya kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za Wananchi.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amekuwa hapa kwenye viwanja vya Ofisi yake Mkoani Arusha kuhakikisha kuwa Mawakili, watumishi wa idara mbalimbali na taasisi zinazotoa misaada ya kisheria zinawajibika kikamilifu kuwasikiliza na kutatua changamoto zote za Wananchi waliojitokeza hapa.

Makonda ameahidi kusimamia kuhakikisha kila mmoja anaridhika na maamuzi yatakayotolewa leo akiahidi pia kutoa msaada wa mawakili kwa kesi zitakazokuwa na uhitaji wa kupelekwa mahakamani.

"Leo nataka niwaambie wananchi wa Arusha hizi siku tatu ni za kwao na ninataka kila mwenye kero aje hapa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wasikilizwe na wataalamu wangu hapa kwaajili ya utatuzi"Alisema

Haya hivyo zoezi hilo limeanza leo Mei 08,2024 na likitarajiwa kukamilika Mei 10, 2024.




Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

YANGA BADO POINTI 2 TU ITANGAZE UBINGWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

DKT NCHIMBI AZURU KABURI LA JOHN KOMBA LITUHI, NYASA

PROF NDAKIDEMI: TULETEENI MIRADI, TUWALIPE NYAMA NA SAMAKI

CHATANDA ANENA MAKUBWA MAADHIMISHO SIKU YA FAMILIA DUNIANI