TAKUKURU YAPONGEZWA KUWA BEGA KWA BEGA NA MBIO ZA SEPESHA ZINAZOPINGA RUSHWA YA NGONO


Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri akizungumza wakati wa uzinduzi wa  mbio za Sepasha Rushwa 2024 zenye Kauli Mbiu ya Acha Rushwa ya Ngono  zitakazofanyika Desemba Mosi jijini Dodoma.


 Shekimweri ameipongeza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa kuziunga kwa asilimia kubwa mbio hizo wakati wa mkutano na vyombo vya habari uliofanyika jijini Dodoma Oktoba 7, 2024.

Kushoto ni Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Dodoma,Eugenius Hazinamwisho na kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Mabalozi wa Sauti ya Wapinga Rushwa (ACVF), Dk. Dinnah Mmbaga. 
Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Dodoma,Eugenius Hazinamwisho akielezea kufurahishwa na mbio hizo zinazosaidia kutoa elimu ya kupiga vita Rushwa ya Ngono.


Mratibu wa mbio hizo, Eliasa Hussein akitoa shukrani kwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Shekimweri kwa kuzilea mbio hizo tangu zilipoanzishwa mwaka 2022. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Mabalozi wa Sauti ya Wapinga Rushwa (ACVF), Dk. Dinnah Mmbaga akielezea jinsi Rushwa ya Ngono inavyoenea katika Taasisi na. Shule na vyuoni.
Baadhi ya maafisa wa TAKUKURU waliohudhuria mkutano huo. 
Mlezi wa Taasisi ya Mabalozi wa Sauti ya Wapinga Rushwa (ACVF), Otieno Rhera akielezea jinsi taasisi hiyo inavyofanya kazi ya kusaidia kutoa elimu ya kupinga rushwa katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo hata kwenye michezo kwa kuandaa mbio hizo za Sepesha Rushwa.
 

Baadhi ya wanahabari na mabalozi wa ACVF.

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
 MSIMAMIZI MKUU 
KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV 
0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.

KIKOSI CHA CBE KIMEWASILI ZENJI KUVAANA NA YANGA

YANGA YAWASILI SALAMA ETHIOPIA

MAYELE AIMWAGIA SIFA LUKUKI YANGA