ZIARA YA DK. NCHIMBI KURINDIMA SIMIYU, SHINYANGA

Na Richard Mwaikenda, Dodoma

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi, Dk. Emmanuel Nchimbi anatarajia kuanza ziara ya siku 6 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga.

Katika ziara hiyo ya kikazi inayoanza kesho Jumapili, DK. Nchimbi ataanbatana na Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Rabia Abdallah Hamid.

Ziara yake itaanza Oktoba 6 katika Mkoa wa Simiyu na kumalizia Shinyanga Oktoba 11, 2024 (kama ratiba Inavyoonesha).

Ziara hiyo ina lengo la kuimarisha uhai wa Chama, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi pamoja na kuhamasisha Wananchi kujitokeza kwa wingi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27, 2024.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.

KAMATI YA UWT KUTOA MSAADA WA KISHERIA NCHINI

KIKOSI CHA CBE KIMEWASILI ZENJI KUVAANA NA YANGA

YANGA YAWASILI SALAMA ETHIOPIA

MAYELE AIMWAGIA SIFA LUKUKI YANGA