HOSPITALI YA BENJAMINI MKAPA MBIONI KUANZISHA KITENGO MAALUMU CHA TIBA KWA WAZEE

Hospitali ya Kanda ya Benjamini Mkapa imeweka mkakati wa kuanzisha matibabu bingwa maalum kwa ajili ya wazee ili kukabiliana na changamoto  mbalimbali za afya za kibingwa zinazolikabili kundi hilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Prof. Abel Makubi  ametoa taarifa hiyo jijini Dodoma Machi 4, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu muelekeo na  mafanikio ya miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Prof.  Makubi amesema kuwa  kutokana na hospitali hiyo kubobea kwenye aina mbalimbali za magonjwa na tafiti wamegundua kuwa kundi la wazee ni miongoni mwa makundi yanayokumbwa na magonjwa  hivyo  umaalum wa matibabu na huduma za afya kiasi cha kuhitaji kitengo maalum cha kibingwa .

Aidha, amebainisha kuwa kutokana na  kuwepo kwa idadi kubwa ya wagonjwa kutoka sehemu mbalimbali kwenda kupata  matibabu kwenye hospitali hiyo, wanatarajia kujenga  hosteli kwa ajili ya kupunguza gharama za wanaowasindikiza kuwauguza
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Prof. Abel Makubi akizungumza katika mkutano huo.
Wanahabari wakiwa katika mkutano huo.

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA

MSIMAMIZI MKUU

KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV

0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

RAIS TRUMP ARARUANA NA RAIS WA UKRAINE

SERIKALI YALIKUBALI OMBI LA DIAMOND

ARAJIGA AULA KOMBE LA DUNIA

MAMBO 8 MWANAMKE HUFANYA KWA MWANAUME ANAYEMPENDA