Mkurugenzi wa Huduma za Upasiaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Rachel Mhavile akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Dkt. Mohamed Janabi katika mkutano na vyombo vya habari katika Idara ya habari, jijini Dodoma Machi 6, 2025, kuelezea mafanikio ya hospitali hiyo kuelekea maadhimisho ya miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Hapa, Dkt. Mhavile akitaja baadhi ya mitambo ya kisasa iliyonunuliwa na MNH kwa lengo la kuboresha huduma za matibabu.
Mtambo wa Angio-Suite
Serikali
imenunua na kusimika mtambo wa kisasa (Angio-Suite) wa Tiba Radiolojia
(Interventional Radiology) uliogharimu
TZS. 2 Bil.ambao umewezesha hospitali kutoa matibabu ya ubingwa bobezi
ambayo yalikuwa hayapatikani hapa nchini na kuongeza idadi ya aina za matibabu
ya kibobezi katika eneo hilo ambapo takribani wagonjwa 2,300 wamehudumiwa tangu
ulipofungwa mwaka 2022. Aidha, kupitia mtambo huo, kwa mara ya kwanza nchini,
Hospitali imefanikiwa kuanzisha huduma mpya za kuweka mirija myembamba
(catheters) kwa kutumia matundu madogo, kutoa damu iliyoganda katika mishipa ya
damu na nyinginezo nyingi ambazo zinafanyika kwa ustadi wa hali ya juu.
2.5.2 Mashine Mpya ya
Mammography
Aidha,
Serikali ilinunua mashine mpya ya
Mammography iliyogharimu TZS 1.8 Bi.
ambayo ina uwezo wa kupima na kutoa picha zinazoweza kugundua uvimbe kwenye
matiti ukiwa katika hatua za awali kabisa. Aidha jumla ya wagonjwa 810,
wamehudumiwa kwa kutumia mashine hiyo tangu iliponunuliwa mwishoni mwa mwaka
2024. Mashine hii ambayo ni kisasa na pekee kwa hospitali za umma, inatumiwa na
madaktari wabobezi wa radiolojia ya wanawake imeleta mapinduzi ya utoaji wa
huduma za uchunguzi wa kisasa kwa wenye magonjwa ya matiti nchini.
2.5.3 Mashine Mpya ta
CT-Scan
Serikali
imeongeza mashine moja ya CT-Scan (dual) iliyogharimu
TZS. 1.8 Bil. yenye uwezo wa vipande 128 hivyo kuongeza idadi ya wagonjwa
wanaopimwa kwa siku kutoka 20 hadi zaidi ya 50 na majibu kupatikana kwa haraka,
kumwezesha daktari kufanya maamuzi mapema na wagonjwa kupata matibabu stahiki
kwa wakati.
2.5.4 Mashine Mpya ya
MRI
2.5.4 Mashine ya
Kidigitali ya X-Ray iliyogharimu kiasi cha TZS. 358 Mil. ambapo
kutokana na uwekezaji huo, Hospitali imefanikiwa kupunguza muda wa kutoa majibu
ya radiolojia (turn-around time) kutoka saa 48 hadi 24 tangu mgonjwa anapopima.
2.5.5 Vifaa vingine
Hospitali
ilifanikiwa kununua vifaa vingine vingi ikiwemo mashine za kusaidia wagonjwa kupumua
18 zilizogharimu kiasi cha TZS. 932 Mil, mashine za endoskopia zilizogharimu
TZS. 215 n.k.
Comments