MATOKEO YA DARASA LA 7 YATANGAZWA

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA)
limetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba uliofanyika kuanzia Septemba 10, 2025. Matokeo hayo yametangazwa leo, Jumatano Novemba 5, 2023, na Katibu Mtendaji wa NECTA, Profesa Said
Ally Mohamed.

Jumla ya watahiniwa 1,172,279 walishiriki katika mtihani huo, ambapo wavulana walikuwa 535,138 sawa na asilimia 45.65, na wasichana 637,141 sawa na
asilimia 54.35. Kiwango cha ufaulu kwa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2025 kimepanda kwa asilimia 0.93.

Watahiniwa 937,581, ambao ni asilimia 81.80 ya 1,146,164 waliofanya mtihani, wamepata madaraja ya
A, B na C. Takwimu hizo zinaonesha ongezeko la ufaulu ukilinganisha na mwaka 2024, ambapo asilimia ya waliofaulu ilikuwa 80.87.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kati ya waliofaulu, wavulana ni 429,104 sawa na asilimia 82.51, na wasichana ni 508,477 sawa na asilimia 81.21.
Pia, NECTA imeeleza kuwa ubora wa matokeo nao umeongezeka. Watahiniwa 422,923 sawa na asilimia
36.90 wamepata madaraja ya juu (A na B), ikilinganishwa na asilimia 35.83 mwaka 2024, hivyo kuonyesha ongezeko la asilimia 1.07. 


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

RAIS SAMIA SIO RAIS JOYCE BANDA WA MALAWI, TANZANIA SIO KENYA

MJUE VIZURI KOCHA MPYA WA YANGA PEDRO

WALIOCHUKUA FOMU CCM ZA KUWANIA USPIKA HAWA HAPA

JESHI LA POLISI LATEKELEZA AGIZO LA RAIS SAMIA, LAONDOA KIZUIZI CHA KUTOTOKA NJE BAADA YA SAA 12 JIONI