MJUE VIZURI KOCHA MPYA WA YANGA PEDRO

 AGE - 49 years


✍️๐ŸฝFalsafa ya Msingi ya Uchezaji

Ni kocha anayeamini katika mpira wa akili(Intelligent Football) usiotegemea nguvu au kasi tu bali ufahamu wa nafasi, mpangilio na uamuzi wa haraka wa matukio.

๐ŸŽจ Mambo Makuu ya Falsafa yake


Kushambulia kwa mpangilio mzuri, kujenga mashambulizi kupitia pasi fupi na kutumia wachezaji wa pembeni kufanya quick transition.


Hapendi timu yake imiliki kwa takwimu tu bali kwa kutengeneza nafasi za maana na kimkakati.


Timu zake zina uwezo mkubwa wa kugeuka kutoka kulinda hadi kushambulia ndani ya sekunde chache.


Timu iikiwa inazuia wachezaji wake wote wanashiriki kujilinda hata washambuliaji wana jukumu la kurudi nyuma pale wakati hawana mpira


Hataki timu yake icheze kwa vurugu ili kushinda haraka bali kwa mpangilio na kujenga utambulisho wao wa kudumu.

✍️๐ŸฝMifumo ya Uchezaji Anayopendelea(Favorite Formations)

Pedro Gonรงalves si kocha anayeshikilia mfumo mmoja pekee yaani “dogmatic”, Anapendelea sana mifumo mitatu.

๐ŸŽจ 4-2-3-1

Huu ulikuwa Mfumo wake maarufu akiwa Angola ambao lengo lake ni kutoa usawa kati ya kuzuia na kushambulia kwa kutumia viungo na washambuliaji wa pembeni.

๐ŸŽจ 4-3-3

Anautumia dhidi ya wapinzani wanaocheza wanaokabia sana juu ili kutoa machaguo mengi zaidi ya pasi na mapana ya uwanja kutoka nyuma kwenda mbele.

๐ŸŽจ 3-4-3 / 3-5-2

Huu anatumia mara nyingi wakati anataka kushambulia kwa tahadhari na kulinda matokeo zaidi. Pia anabadilika muundo na majukumu ya wachezaji kulingana na mwenendo wa mechi.

✍️๐ŸฝVitu gani natarajia kuona akiongeza Young Africans? ๐Ÿ”ฐ

1-Mabadiliko ya muundo wa ushambuliaji wenye mpangilio mzuri kutoka chini

2-Kuimarika kwa muundo wa uzuiaji kitu kinachoweza kuwalipa kwenye mechi kubwa zneye presha hasa za CAF CL.

3-Kuinua ubora kwa baadhi ya Wachezaji wa Young Africans.


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

WALIOCHUKUA FOMU CCM ZA KUWANIA USPIKA HAWA HAPA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

RAIS SAMIA SIO RAIS JOYCE BANDA WA MALAWI, TANZANIA SIO KENYA

MATOKEO YA DARASA LA 7 YATANGAZWA

JESHI LA POLISI LATEKELEZA AGIZO LA RAIS SAMIA, LAONDOA KIZUIZI CHA KUTOTOKA NJE BAADA YA SAA 12 JIONI