MECHI ZA YANGA KLABU BINGWA AFRIKA KUFANYIKA AMAAN ZANZIBAR

Timu ya Yanga imeamua kutumia Uwanja wa New Amaan Complex,  Zanzibar kwa michezo yake ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Dar es Salaam, Afisa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe, amesema uamuzi huo umetokana na tathmini ya kina iliyofanywa na uongozi wa klabu baada ya droo ya hatua ya makundi kupangwa.

Yanga imepangwa katika Kundi B ikichuana na vigogo wa soka barani Afrika ambao ni Al Ahly ya Misri, AS FAR Rabat ya Morocco na JS Kabylie ya Algeria.

“Kundi hili ni miongoni mwa makundi magumu zaidi. Kwa lugha ya mpira, ni kundi la kifo. Hakuna timu nyepesi, yeyote anaweza kufuzu robo fainali,” amesema Kamwe.

Ameongeza kuwa Klabu ya Yanga tayari imeanza maandalizi kuhakikisha inakuwa miongoni mwa timu mbili zitakazofuzu hatua ya robo fainali.

 “Tutaanzia mchezo wa kwanza nyumbani dhidi ya FAR Rabat, kisha tutasafiri kwenda Algeria kucheza na JS Kabylie. Michezo yetu mitatu ya nyumbani tutacheza New Amaan Complex, Zanzibar,” amefafanua Kamwe.

Aidha, amewataka mashabiki wa soka visiwani Zanzibar kujiandaa kuipokea na kuipa sapoti timu hiyo katika safari yake ya kutafuta mafanikio barani Afrika.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

RAIS SAMIA SIO RAIS JOYCE BANDA WA MALAWI, TANZANIA SIO KENYA

MJUE VIZURI KOCHA MPYA WA YANGA PEDRO

WALIOCHUKUA FOMU CCM ZA KUWANIA USPIKA HAWA HAPA

JESHI LA POLISI LATEKELEZA AGIZO LA RAIS SAMIA, LAONDOA KIZUIZI CHA KUTOTOKA NJE BAADA YA SAA 12 JIONI