BINTI WA KITANZANIA GLORIA MAJULE ASHINDA TUZO YA UANDISHI BORA WA FILAMU YA MALARIA MAREKANI ‎

Binti wa Kitanzania, Gloria Majule, ambaye ni mtoto wa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, Dkt. Neema Majule, amepata mafanikio makubwa baada ya kutwaa tuzo ya Uandishi Bora wa Filamu kuhusu Malaria nchini Marekani.


‎Gloria, ambaye anasoma katika Chuo Kikuu cha Cornell nchini Marekani na tayari ana shahada mbili, aliibuka mshindi wa tuzo hiyo kwa mwaka 2025/2026 baada ya kuwashinda washiriki zaidi ya 1,000 kutoka mataifa mbalimbali. Ushindi huo ulimwezesha kutembea kwenye zulia jekundu (Red Carpet) kama sehemu ya hafla ya utoaji wa tuzo.


‎Kupitia mafanikio hayo, Gloria ameendelea kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa. Mabango yanayotangaza ushindi wake na filamu hiyo yamewekwa katika maeneo mbalimbali jijini New York, Marekani.


‎Filamu hiyo, inayoangazia ugonjwa wa malaria ambao unaendelea kuathiri kwa kiasi kikubwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, ikiwemo Tanzania, imepata umaarufu mkubwa nchini Marekani na kuvutia watazamaji wengi.


‎Kwa mujibu wa taarifa hizo, Gloria ameandika historia kwa kuwa Mwafrika wa pili kushinda tuzo hiyo ya kimataifa ya uandishi wa filamu.





 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DK MAGUFULI ATANGAZA KIAMA CHA MAJAMBAZI, WEZI NA MAFISADI KATIKA MIKUTANO YA KAMPENI SUMBAWANGA,TUNDUMA, ILEJE NA MBOZI

MAAFISA JENERALI WASTAAFU 17 WA JWTZ WAAGWA.

PICHA YA RAIS ILIYOBAMBA WIKI HII

JUA AINA NNE ZA KABILA LA WASUKUMA

18 WAPITISHWA KUGOMBEA UONGOZI YANGA

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

VIONGOZI BORA BARANI AFRIKA KWA SASA.