DKT. MAJULE AWATAKA WANAWAKE KUGOMBEA UONGONGOZI, KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI

Na Mwandishi Wetu, Mpwapwa

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, Dk. Neema Peter Majule, amewataka wanawake nchini kujitokeza kwa wingi kushiriki nafasi za uongozi na kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi ili kuongeza mchango wao katika maendeleo ya taifa.

Dk. Majule ambaye pia nia Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma, alitoa kauli hiyo Julai 25, 2026, alipokuwa mgeni rasmi katika tamasha la Mpwapwa Women Gala lililofanyika katika Ukumbi wa CCM wilayani Mpwapwa, mkoani Dodoma.


‎Alisema wanawake wanapaswa kutumia mazingira wezeshi yaliyopo kujikwamua kiuchumi kupitia shughuli za uzalishaji na ujasiriamali, huku wakijitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ili kuongeza idadi ya wanawake katika vyombo vya maamuzi kuanzia ngazi za chini hadi kitaifa.


‎"Ni wakati wa wanawake kutumia fursa zilizopo kujenga uchumi wao na kushiriki kikamilifu katika uongozi kwa maendeleo ya jamii na taifa," alisema Dk. Majule.


‎Tamasha hilo liliandaliwa mahsusi kuwatambua na kuwapongeza wanawake kwa mchango wao katika maendeleo ya Wilaya ya Mpwapwa kwa mwaka 2025/2026.


‎Katika hafla hiyo, wanawake waliofanya vizuri katika sekta mbalimbali walitunukiwa zawadi ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao na kuhamasisha utendaji bora zaidi. Sekta zilizotambuliwa ni pamoja na afya, elimu, kilimo na nyinginezo, ambapo wauguzi, walimu, wakulima na wanawake wengine waliotoa mchango mkubwa walipokea tuzo na zawadi.


‎Washiriki wa tamasha hilo walieleza kuwa Mpwapwa Women Gala imekuwa jukwaa muhimu la kuhamasisha mshikamano wa wanawake, kutambua juhudi zao katika maendeleo na kuibua ari ya kushiriki zaidi katika shughuli za kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Dkt. Majule (wa nne kushoto) akiwa na baadhi ya washiriki kwenye kongamano hilo.







Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

Soma Taarifa ya UTEUZI:Rais Jakaya Kikwete amemteua Dkt. Ben E. Moshi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya PUMA Energy (zamani ilijulikana kama BP Ltd)

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

MAAFISA JENERALI WASTAAFU 17 WA JWTZ WAAGWA.

PICHA YA RAIS ILIYOBAMBA WIKI HII

18 WAPITISHWA KUGOMBEA UONGOZI YANGA

JUA AINA NNE ZA KABILA LA WASUKUMA

BINTI WA KITANZANIA GLORIA MAJULE ASHINDA TUZO YA UANDISHI BORA WA FILAMU YA MALARIA MAREKANI ‎

DK MAGUFULI ATANGAZA KIAMA CHA MAJAMBAZI, WEZI NA MAFISADI KATIKA MIKUTANO YA KAMPENI SUMBAWANGA,TUNDUMA, ILEJE NA MBOZI