Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya Mh.Dormohamed Issa leo Julai 22 2026 ametembelea eneo linalotarajiwa kujengwa uwanja wa mpira wa timu ya Mbeya City Fc.
Eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ya hekari saba unatarajiwa kujengwa uwanja wa mpira wa miguu ,michezo mingine sambamba na maeno ya biashara.
Maandalizi ya hatua za awali za ujenzi wa uwanja huo yameanza kwa zoezi la usawazishaji wa eneo. Awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya Bw.Justice Kijazi alitoa maelekezo kwa waandisi wa Jiji la Mbeya kuandaa ramani ya uwanja na kuzungushia uzio eneo hilo.


Comments