MISRI YAZINDUA MAKAO MAKUU MAKUBWA ZAIDI YA KIJESHI DUNIANI


Misri imezindua Makao Makuu Makubwa zaidi ya Kijeshi Duniani, yakiipita Pentagon ya Marekani.

Himaya mpya ya Wizara ya Ulinzi ya Misri, inayojulikana kama Octagon si kikubwa zaidi barani Afrika tu, bali pia imeipita Pentagon ya Marekani na kuwa kituo kikubwa zaidi cha makao makuu ya ulinzi duniani.

Makao hayo Makuu ya amri ya Serikali yanatumika pia kama Wizara ya Ulinzi ya Misri mradi unaowakilisha hatua kubwa ya uhuru kwa vikosi vya jeshi vya nchi hiyo.

Mji huo mkuu mpya wa jeshi la Misri upo jangwani yapata kilomita 45 mashariki mwa Cairo ukiwa na ukubwa wa takriban hekari 22,000, na eneo la sakafu la zaidi ya futi za mraba milioni 50.5.

Eneo hilo lina majengo manane ya umbo la pembe nne (yanayojumuisha Jeshi, Jeshi la Wanamaji, Jeshi la anga na Ulinzi wa anga) na ni kituo cha amri kilichojengwa ili kuhifadhi taasisi muhimu za eneo hilo zima.



 


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DK MAGUFULI ATANGAZA KIAMA CHA MAJAMBAZI, WEZI NA MAFISADI KATIKA MIKUTANO YA KAMPENI SUMBAWANGA,TUNDUMA, ILEJE NA MBOZI

VIONGOZI BORA BARANI AFRIKA KWA SASA.

ZIJUE SIFA ZA WANYAKYUSA WA KYELA NA RUNGWE

18 WAPITISHWA KUGOMBEA UONGOZI YANGA

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

PICHA YA RAIS ILIYOBAMBA WIKI HII

UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MSALATO DODOMA KUANZA KUTUMIKA SEPTEMBA 2026