RAIS SAMIA AMTEUA BOSS WA TSN KUWA MKURUGENZI MKUU WA TBC. RAIS SAMIA AMTEUA BOSS WA TSN KUWA MKURUGENZI MKUU WA TBC.
Rais Samia Suluhu Hassan, amemteua Asha Dachi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, kabla ya uteuzi huo Dachi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN).
Anachukua nafasi ya Dkt. Ayub Rioba Chacha ambaye amemaliza muda wake wa uongozi.
Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu leo Julai 14, 2026.

Comments