Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), akibainisha kuwa zaidi ya shilingi trilioni 6 zimetengwa kwa ajili ya mradi huo mkoani Kigoma. Uwekezaji huo ni mkakati thabiti wa serikali wa kuufungua kiuchumi mkoa wa Kigoma na maeneo ya jirani pamoja na nchi jirani za DR. Congo na Burundi..
Kukamilika kwa reli hiyo kutaleta mapinduzi makubwa ya usafiri, ambapo safari ya kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma itakayochukua saa 8 pekee kwa SGR, tofauti na zaidi ya saa 24 kwa barabara au siku mbili kwa treni ya zamani. Mabadiliko hayo yatafungua fursa mpya za biashara, uwekezaji, na usafirishaji kwa wakazi wa mkoa huo na maeneo yote ya magharibi mwa Tanzania
'
Comments