Mwigombe Technical Secondary School, Kijijini Kiriba, Musoma Vijijini
Wanakijiji wakishirikiana na Wazaliwa wa Kijiji cha Kiriba, Jimbo la Musoma Vijijini, wanaendelea na ujenzi wa sekondari ya ufundi ambayo itawekewa Jiwe la Msingi na Mwenge wa Uhuru tarehe 8.8.2026
Michango ya ujenzi wa sekondari hiyo:
(i) Wanakijiji
(ii) Familia Mashenene
(iii) Baadhi ya wazaliwa wa Kata ya Kiriba
(iii) Mbunge Prof Muhongo
(iv) Wadau wa Maendeleo: benki za CRDB & NMB
Miundombinu itakayokuwa imekamilika ifikapo tarehe 4.8.2026
(i) Jengo lenye vyumba 2 vya madarasa na ofisi 1 katikati
(ii) Jengo lenye nyumba 2 vya madarasa
(iii) Choo chenye matundu 5
Ujenzi unaendelea kwa kasi kubwa ili sekondari hiyo ifunguliwe Januari 2027.
Alhamisi, 6.8.2026: Sherehe Kijijini Kiriba, Kata ya Kiriba
Wanakijiji wa Kijiji cha Kiriba watafanyiwa sherehe na Mbunge wao, Prof Sospeter Muhongo ikiwa ni kuwapongeza kwa juhudi zao za kujitolea kuchangia maendeleo yao wakishirikiana na Serikali yetu
Mafanikio yatakayosherehekewa:
(i) Ujenzi wa Sekondari ya Ufundi ya Mwigombe kijijini hapo
(ii) Ujenzi wa Zahanati mpya kijijini hapo. Serikali imechangia Tsh 259,000,000 (Tsh 259m), na Wanakijiji wamechangia nguvukazi
Shukrani:
Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini na Viongozi wao wa ngazi zote wanaendelea kuishukuru sana Serikali yetu chini ya uongozi mzuri wa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kugharamia miradi ya maendeleo ya Jimboni mwetu - ahsante sana.
Picha zilizoambatanishwa hapa zinaonesha ujenzi unaoendelea kwenye Mwigombe Technical Secondary School ya kijijini Kiriba, Kata ya Kiriba, Musoma Vijijini
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
P. O. Box 6
Musoma
Date: Fri, 31.7.2026
Comments