LAAC YAZIONYA HALMASHAURI KUPUUZA, KUDHARAU HOJA ZA KAMATI ZA BUNGE, CAG

 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Ado Shaibu, amezionya Halmashauri za wilaya nchini kuacha tabia ya kudharau na kupuuza hoja na maelekezo ya kamati hiyo na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Ametoa onyo hilo alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari baada ya kamati hiyo kufanya kikao na viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Same jijini Dodoma Agosti 20, 2026.

Akisoma tamko la kamati, Shaibu amewataka viongozi hao kutekeleza maagizo yote ya CAG na yale yanayotolewa na Kamati yake. Hadi jana Agosti 20 kamati hiyo imehoji halmashauri 36 bado 3 watakazomalizia leo Agosti 21. Kwa upande wa Halmashauri ya Same amewarudisha kwenda kutekeleza na wataitwa tena kujiridhisha kama maagizo hayo yote yametekelezwa kama kamati hiyo ilivyoagiza.
"Ifahamike kwamba kamati yake inafanya kazi kwa niaba ya bunge, kuidharau kamati hiyo ni swa na kulidharau bunge kitu ambacho hakikubaliki hata kidogo,"amesema Shaibu.




Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Ado Shaibu akizungumza na vyombo vya habari katika kikao hicho.

Wabunge ambao ni wajumbe wa kamati hiyo wakiwa katika kikao hicho.







Mmoja wa viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same akijibu hoja.


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

OWM–TAMISEMI YASHINDA TUZO YA MABADILIKO YA KIDIJITALI KATIKA TEHAMA AWARDS 2026

Soma Taarifa ya UTEUZI:Rais Jakaya Kikwete amemteua Dkt. Ben E. Moshi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya PUMA Energy (zamani ilijulikana kama BP Ltd)

VIONGOZI NA WATENDAJI WA MATAWI UVCCM PANGANI WANOLEWA

NMB YAWAUNGANISHA WANANCHI NA HUDUMA, FURSA ZANZIBAR

HIZI HAPA TAKWIMU ZA PETER SHALULILE MCHEZAJI MPYA WA YANGA SC 🔰 🔥