Makundi maalumu 27,946 yamesajiliwa kwenye mfumo wa NeST na kupata zabuni zenye jumla ya thamani ya Shilingi Bilioni 56, kupitia Mfumo huo.makundi ya vijana ni 13, 317 wanawake 13,400, wazee 643 na watu wenye ulemavu 586.
Hayo yemebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Dennis Simba wakati wa mkutano na vyombo vya habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO, katika Mji wa Serikali wa Mtumba jijini Dodoma, Agosti 20, 2026.
Sheria ya Ununuzi wa Umma, imezielekeza taasisi zote za umma kutenga asilimia 30 ya bajeti zao za ununuzi kwa ajili ya makundi maalum (vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu).
Lengo la PPRA, kwa kuzingatia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo
2050, ni kuwa na takribani makundi 300,000 yaliyo tayari kuomba zabuni. Hatua hii
ni sehemu ya jitihada za Serikali kutoa ajira na kazi kwa Watanzania ambao
hawana uwezo wa kuwa na kampuni, ambao wanaweza kujiunga kwenye vikundi na
kutekeleza zabuni husika. ร Riple effect ya
kazi na ajira 3,000,000
Kutokana na nia ya kuwainua Watanzania kiuchumi, Kundi maalum linaweza
kupata zabuni moja yenye thamani ya hadi Shilingi Milioni 500.
Kutokana na umuhimu wa suala hili, Serikali imeliweka kuwa sehemu ya
ajenda muhimu kwenye Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka huu. Hatua
iliyoongeza usajili wa vikundi, hamasa na utekelezaji wa utoaji wa zabuni. Na
hapa nichukue fursa hii kuishukuru Ofisi ya Rais – Wizara ya Maendelea ya
Vijana kwa kuridhia ombi letu la kushhirikiana nao kwenye jambo hili ambapo
tutazunguka nao katika Halmashauri zote 184 nchini.
Hivyo, tunawasihi Watanzania tuendelee kujiunga kwenye vikundi vya watu
watatu na kuendelea, kuvisajili kwenye Halmashauri zao, na kisha wasajili kwenye
Mfumo wa NeST ambao ndio wenye zabuni zote za umma. Lengo kuu ni kuhakikisha
kuwa tunakuwa na uchumi jumuishi; kwamba kila Mtanzania ananufaika na
anachangia pia kwenye ukuaji wa uchumi katika ngazi yoyote aliyopo.
Comments