Jumamosi Jioni Mwenyekiti wa Kamati ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mh. Deo Mwanyika akiwa katika matukio mbalimbali alipohudhuria maadhimisho ya siku 365 za Mama SSH kwenye sekta ya kilimo yaliyofanyika Ukumbi wa Mlimani City. Shughuli hiyo iliambatana na futari iliyoandaliwa na Mh Waziri Hussein Bashe. Vilevile vijana 10 vya vyuo vikuu walioshinda katika maandiko yaliyotoa suluhisho katika changamoto mbalimbali za kilimo walizawadiwa vyeti na fedha. Picha mbalimbali za tukio hilo.
- Get link
- Other Apps