BREAKING NEWZZZZZ GURUMO ALAZWA MUHIMBILI

Kamanda Muhidin Maalim Gurumo

Na Ras Makunja,
Kamanda wa FFU Ughaibuni

Mwanamziki Muhidin Gurumo Kalazwa Hosptalini Muhimbili
ward ya Mwaisela Na.5
Mwanamziki mkongwe wa muziki wa dansi Muhidin Maalimu Gurumo
alimaarufu kama Anko,kiongozi wa bendi ya Msondo Ngoma, amelazwa katika hosptali ya Muhimbili,ward ya Mwaisela namba 5 akiwa anasumbuliwa na matatizo ya mapafu kujaa maji.

Mzee Muhidin Gurumo ni baba mwanzilishi wa bendi ya Nuta Jazz ambayo sasa "Msondo Ngoma Music Band" aka Baba wa Mziki, aka Mambo hadharani.

Anko Muhidini Maalimu Gurumo amekuwa katika medani ya mziki kuanzia mwishoni mwa miaka ya 1950s rasmi mwaka 1960 na akiwa moja ya wanamziki wanzilishi wa Nuta jazz band 1964, kabla ya kubadili jina na kuitwa JUWATA JAZZ ikiwa chini ya chama cha wafanyakazi.

Anko Gurumo ni mwanamziki mtunzi,mwimbaji mkongwe na mbunifu wa mtindo mbali ya dansi kama vile Msondo Ngoma, Sikinde Ngoma ya Ukae (alipokuwa Mlimani Park) na Ndekule (alipohamia kwa muda Orchestra Safari Sound wana OSS) n.k yeye akiwa ndie anayetoa majina haya.

Mzee Gurumo ni Baba wa mziki wa dansi nchini na pamoja kuwa amewahi kupigia bendi nyingi lakini "Msondo Ngoma Music Band" ndiyo ngome yake.

Ras Makunja na Globu ya Jamii inamwomba Mwenyezi Mungu ampe afueni Kamanda wetu Mzee Gurumo. Na pia wadau wa muziki tujitokeze kumsaidia

 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI