MUBARAK APELEKWA HOSPITALI CAIRO

Hosni Mubarak

Aliyekuwa Rais wa Misri, Hosni Mubarak, anatarajiwa kupelekwa kwenye hospitali ya kijeshi mjini Cairo baada ya daktari kutangaza kuwa afya yake inamruhusu kusafiri.
Amekuwa hospitalini huko Sharm el-Sheikh tangu aanze kuumwa wakati wa kuhojiwa juu ya madai ya kuhusishwa na rushwa na mauaji ya waandamanaji.
Waendesha mashtaka walisema Bw Mubarak mwenye umri wa miaka 82 alitakiwa kupelekwa hospitali ya magereza ya Tora, lakini haikuwa tayari kumpokea.
Baraza la kijeshi lililoshikilia madaraka mwezi Februari linashinikizwa kumshtaki.
Watoto wawili wa kiume wa Bw Mubarak, Gamal na Alaa, pamoja na maafisa wengine waandamizi na wafanyabiashara walio karibu naye tayari wameshikiliwa kwenye gereza la Tora.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE