Waziri Mkuu Mizengo Pinga akiangalia zawadi ya chombo cha kuwekea sukari aliyopewa na Naibu waziri wa Utamaduni wa China, Zhao Shaohua wakati naibu waziri huyo alipomtembelea ofisini kwake jana mjini Dodoma. Zhao pamoja na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku nne ikiwa na malengo ya kuimarisha mahusiano ya kiutamaduni baina ya Tanzania na China.
Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Utamaduni, Anjela Ngovi akimvalisha kanga Naibu Waziri wa Utamaduni wa China, Zhao Shaohua wakati naibu waziri huyo alipotembelea mjini Dodoma jana, kwa ajili ya kuonana na viongozi wa Serikali huku Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi (katikati) na Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni, Prof. Helmasi Mwansoko (kulia) wakishuhudia.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Emmanuel Nchimbi (kulia) akisalimiana na Naibu Waziri wa Utamaduni wa China, Zhao Shaohua (katikati) katika Uwanja wa Ndege wa mjini Dodoma,Kulia ni Zhao Haisheng aliyeambatana na ujumbe huo.
(PICHA ZOTE NA ANNA NKINDA-MAELEZO)
Comments