Mwizi mmoja nchini Uchina alitoka mbio baada ya kufanya wizi, kiasi kwamba wanariadha wanamtaka mwizi huyo kwa ajili ya mbio fupi.
China
China wanataka kutumia uzoefu wa mwizi kuwa mwanariadha..
Mwizi huyo, Lei Pai, alionekana akikimbia mita mia moja na kumi kwa muda wa sekunde kumi na moja, baada ya kukwapua betri.
Picha za mwizi huyo akikimbia zilionekana katika kamera za ulinzi, maarufu kama CCTV.
"Ukizingatia alikuwa amevaa viatu vya kawaida na kasi aliyokimbia" amesema kocha wa riadha wa jimbo la Zhengzhou. Nadhani atatufaa sana, iwapo akielekezwa jinsi ya kukimbia na akipatiwa vifaa vinavyotakiwa, amesema kocha huyo wa jimbo la Henan.
Comments