UINGEREZA KUISAIDIA KENYA SOMALIA

David Cameron ametangaza kuwa meli zilizosajiliwa Uingereza zinaweza kuwa na walinzi waliojihami ili kujikinga na maharamia.
David Cameron


Akihojiwa na BBC, Waziri Mkuu wa Uingereza alisema anataka kushughulikia zaidi tishio linalokabili meli katika pwani ya Somalia - ambako meli 49 zilitekwa na maharamia mwaka jana.

Hivi sasa sheria hairuhusu walinzi kubeba silaha kwenye meli za Uingereza, lakini Bwana Cameron alisema anakusudia kubadilisha sheria hiyo:

"Sasa tutasema kwamba meli zilizosajiliwa Uingereza, zitaweza kuwa na walinzi wenye silaha katika meli hizo zikitaka.

Mimi nataka kuhakikisha kuwa maharamia wengi zaidi wanafikishwa mahakamani; na nataka tuitazame zaidi nchi hii ya Somalia iliyoharibika...na vipi tunaweza kujaribu kushughulikia sababu za utekaji nyara, uharamia, kikombozi, na matatizo yote yanayotokana na nchi hii iliyochafuka."


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

NCHIMBI AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA