MAPADRI WALIOKUFA KWA AJALI WAOMBEWA DAR

Baadhi ya waumini wakilia wakati majeneza yenye miili ya mapadri na Mlei mmoja ikipakiwa kwenye magari baada ya kuombewa.


0934

Mapadri wakiwa wamebeba moja ya majeneza yenye miili ya mapadri watatu na kijana mlei wakipeleka kwenye gari kwenda kuhifadhiwa vizuri Hospitali ya Agakhan, baada ya kuiombea katika ibada maalumu iliyofanyika jana Kanisa la Katoliki Msimbazi, Dar es Salaam, tayari kusafirishwa nchini kwao Italia kwa mazishi. Walikufa katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Kongwa kwenda Dar es Salaam, iliyotokea hivi karibuni eneo la Ruvu, Pwani, baada ya kugongana uso kwa uso na lori.

Askofu Mkuu Msaidizi wa Kanisa la Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Salutaris Libena akiiombea miili ya mapadri watatu na kijana mlei katika ibada maalumu iliyofanyika jana Kanisa la Katoliki Msimbazi, Dar es Salaam, tayari kusafirishwa nchini kwao Italia kwa mazishi. Walikufa katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Kongwa kwenda Dar es Salaam, iliyotokea hivi karibuni eneo la Ruvu, Pwani, baada ya kugongana uso kwa uso na lori. Picha zaidi uk 14.

Comments

JigambeAds said…
Mungu azilaze pema roho zao . Amen!

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI