Mmoja wa madiwani akitoa shukrani baada ya mkutano huo kufunguliwa
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza (kulia) akihutubia wakati wa uzinduzi wa mafunzo kwa ajili ya uanzishaji wa wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF/TIKA), kwa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, mjini Kibaha. Kutoka kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Hamis Mdee na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Jenifa Omole.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza (kushoto) akiagana na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Hamis Mdee, mara baada ya kupiga picha na viongozi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa ajili ya uanzishaji wa wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF/TIKA) katika Halmashauri hiyo, mjini Kibaha
Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa gazeti la Jambo Leo, Grace Michael akijitambulisha katika mkutano huo
Mmoja wa madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha,akitambulisha wakati wa mkutano huo
Baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha wakiwemo madiwani, wakihudhuria mafunzo hayo.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Hamis Mdee (kushoto), akielezea umuhimu wa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF/TIKA), wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa ajili ya uanzishaji wa wa Mfuko huo kwa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, mkoani Pwani jana.Kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Jenifa Omole.
Comments