Katibu wa
Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimkabidhi cheti
mhitimu wa kidato cha sita, Burilo Busagi, katika mahafali ya kidato cha sita
shule ya Sekondari Nsumba, Mwanza. Jumla ya wahitimu 374 wa kidato hicho
walipewa vyeti. Kushoto ni Mkuu wa shule hiyo Josephat Zakeyo.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na
Uenezi Nape Nnauye akimkabidhi cheti mhitimu wa kidato cha sita, Tifugundulwa
Tumbika katika mahafali ya kidato cha sita shule ya Sekondari Nsumba, Mwanza.
Tumbika alikabidhiwa cheti hicho kwa kuibuka mwanafunzi bora katika kuzungumza
Kiingereza. Wapili kulia ni Mkuu wa shule hiyo Josephat Zakeo.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi
na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na mwanafunzi aliyesoma shule ya sekondari ya
Nsumba, Mwanza, kati ya mwaka 1954 na 1957 (darasa la nane na kumi) Damas Ngoma,
wakati wa mahafali ya kidato cha sita ya shule hiyo leo. Nape ambaye alikuwa
mgeni rasmi katika mahafali hayo alisoma pia katika shule hiyo hadi kidato cha
nne mwaka ambako alimaliza mwaka 97. Watatu ni Mkuu wa shule hiyo Josephat
Zakeo.(Picha zote na Bashir Nkoromo).
Comments