Shinikizo dhidi ya Syria laongezeka

Mataifa ya magharibi yanajiandaa kupigia debe azimio kali kwenye mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na mgogoro uliopo nchini Syria.

Katibu mkuu wa muungano wa Mataifa ya Kiarabu Nabil al-Arabi anatarajiwa kutoa ombi kwa Baraza la Usalama kuunga mkono mpango mpya wa muungano huo unaotaka rais wa Syria Bashar al-Assad ajiuzulu.

Afisa mmoja kutoka wizara ya mashauri ya nchi za kigeni ya Syria amesema kuwa Syria 'itashinda sera za kuzua vurugu', shirika la habari linalomilikiwa na serikali Sana limesema.

"Tunasikitika kwamba matamshi kama hayo bado yanatolewa na mataifa yaliyo na mazoea ya kufanya eneo la Mashariki ya Kati kuwa uwanja wa kuonyesha upumbavu wao pamoja na majaribio yao yasioleta manufaa," afisa huyo akaongeza.

Mpango huo uliopendekeza na muungano wa nchi za Kiarabu na kuungwa mkono na Marekani, Uingereza na Ufaransa, unaotoa wito kwa Bw. Assad kukabidhi madaraka kwa naibu wake ambaye ataunda serikali ya muungano wa kitaifa.

Moscow imesema kuwa mpango huo "hauna usawa" na "utatoa mwanya'' wa uingiliaji wa maswala ya ndani ya Syria.

Ikulu ya White House ilisema Jumatatu kwamba bwana Assad alikuwa ameshindwa kuidhibiti Sria na kuongeza kuwa sharti ''ataondoka''

Marekani imetoa wito kwa mataifa yote kutoa msimamo wao kuhusiana na kile ilichokitaja kuwa udhalimu serikali ya Syria.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA