Ajali yauwa mshauri wa Kabila

Mshauri mwandamizi wa Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, amekufa kwenye ajali ya ndege.

Mshauri huyo, Augustin Katumba Mwanke, alikufa pamoja na rubani, wakati ndege hiyo ya kibinafsi ilipuanguka karibu na mji wa Bukavu, kusini mwa nchi.

Waziri wa Fedha, Augustin Matata Ponyo, na abiria wengine walijeruhiwa vibaya.

Augustin Matata Ponyo, gavana wa Kivu Kusini, Marcellin Cishambo Rohuya, na mshauri mwengine wa rais, Antoine Ghonda, inaarifiwa waliumia vibaya.

Ndege hiyo ilikuwa inasafiri kutoka Kinshasa kuelekea Kivu.

Sababu ya ajali hiyo haijulikani.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA

Wasifu wa Kizza Besigye

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda