ANC yakwepa uamuzi kuhusu Malema

Chama tawala cha Afrika Kusini, ANC, kimeamua kutekeleza uamuzi wa awali wa kusimamisha uanachama wa kiongozi wa tawi la vijana la chama, Julius Malema.
Hata hivo, kamati ya rufaa ya chama imeamua kuiomba kamati ya maadili kuzingatia tena muda wa kumtoa Bwana Malema chamani.

Kamati hiyo imesema inampa Bwana Malema fursa ya kujitetea tena kama anaona adhabu aliyopewa ni kubwa mno.

Uamuzi wa kumtoa katika chama kwa muda wa miaka 5, ulifikiwa mwezi Novemba, baada ya kukutikana kuwa ameleta aibu kwa chama, kwa kumuendea kinyume Rais Zuma; na kutoa wito kuwa serikali ya Botswana, nchi jirani, inafaa kubadilishwa.

Bwana Malema ameushutumu uongozi wa ANC kuwa unawadharau maskini wa Afrika Kusini, ambao ndio waliompatia ushindi Rais Zuma kwenye uchaguzi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA

UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MSALATO DODOMA KUANZA KUTUMIKA SEPTEMBA 2026

Wasifu wa Kizza Besigye

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA