ANC yakwepa uamuzi kuhusu Malema

Chama tawala cha Afrika Kusini, ANC, kimeamua kutekeleza uamuzi wa awali wa kusimamisha uanachama wa kiongozi wa tawi la vijana la chama, Julius Malema.
Hata hivo, kamati ya rufaa ya chama imeamua kuiomba kamati ya maadili kuzingatia tena muda wa kumtoa Bwana Malema chamani.

Kamati hiyo imesema inampa Bwana Malema fursa ya kujitetea tena kama anaona adhabu aliyopewa ni kubwa mno.

Uamuzi wa kumtoa katika chama kwa muda wa miaka 5, ulifikiwa mwezi Novemba, baada ya kukutikana kuwa ameleta aibu kwa chama, kwa kumuendea kinyume Rais Zuma; na kutoa wito kuwa serikali ya Botswana, nchi jirani, inafaa kubadilishwa.

Bwana Malema ameushutumu uongozi wa ANC kuwa unawadharau maskini wa Afrika Kusini, ambao ndio waliompatia ushindi Rais Zuma kwenye uchaguzi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA