BBC YAANZA KUFUNDISHA UANDISHI WA HABARI KWA LUGHA YA KISWAHILI

Waandishi wa habari wa BBC



Chuo cha Uandishi Habari cha BBC (BBC College of Journalism ) kwa kushirikiana na Idhaa ya Dunia ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC World Service) wanafurahia kuzindua mwongozo maalum wa uandishi wa habari katika lugha Kiswahili.

Kiswahili ni miongoni mwa lugha sita zinazohusika na awamu hii, nyingine ni kiindonesia, kipashto, kiuzbek, kiazeri na kikyrgyz.

Matoleo haya mapya yanaongeza lugha zaidi ya zile ambazo tayari zilizindua mwaka mmoja uliopita: kiarabu, kichina, kiurdu, kirusi na kifaransa.

Miongozo hii inatumia uzoefu mkubwa na utaalam wa miaka mingi kutoka miongoni mwa waandishi wa BBC, na sasa tunayo furaha kuweza kutoa fursa kwa waandishi wa habari kote duniani kunufaika kwa utaalam huu.

Miongozo hii inatoa msisitizo kuhusu, pamoja na mengine yote, jinsi gani uandishi wa habari unategemea sana lugha kujitosheleza.

Kuweza kujadili misingi ya uandishi habari, inabidi kwanza kuelewa nafasi ya lugha katika kubainisha mawazo fulani katika misingi hiyo.

Hii ni hatua ya kwanza, tungependa kurasa hizi zikiongezeka na kuwa miongozi kamili ya uandishi habari na lugha.

Pata maelekezo jinsi ya kutumia

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA

UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MSALATO DODOMA KUANZA KUTUMIKA SEPTEMBA 2026

Wasifu wa Kizza Besigye

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA