| ||||
Kiswahili ni miongoni mwa lugha sita zinazohusika na awamu hii, nyingine ni kiindonesia, kipashto, kiuzbek, kiazeri na kikyrgyz. Matoleo haya mapya yanaongeza lugha zaidi ya zile ambazo tayari zilizindua mwaka mmoja uliopita: kiarabu, kichina, kiurdu, kirusi na kifaransa. Miongozo hii inatumia uzoefu mkubwa na utaalam wa miaka mingi kutoka miongoni mwa waandishi wa BBC, na sasa tunayo furaha kuweza kutoa fursa kwa waandishi wa habari kote duniani kunufaika kwa utaalam huu. Miongozo hii inatoa msisitizo kuhusu, pamoja na mengine yote, jinsi gani uandishi wa habari unategemea sana lugha kujitosheleza. Kuweza kujadili misingi ya uandishi habari, inabidi kwanza kuelewa nafasi ya lugha katika kubainisha mawazo fulani katika misingi hiyo. Hii ni hatua ya kwanza, tungependa kurasa hizi zikiongezeka na kuwa miongozi kamili ya uandishi habari na lugha. Pata maelekezo jinsi ya kutumia |
Waandishi wa habari wa BBC
Comments