JK, SPIKA KUHUDHURIA MAADHIMISHO YA SHERIA.
RAIS Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini, yatakayo fanyika kitaifa katika viwanja vya Mahakama ya Rufaa jijini Dar es salaam.
Akizungumza na Waandishi wa habari jana Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman alisema maadhimisho hayo yamelenga katika kujadili masuala mbalimbali ya kisheria ili kuweza kutoa elimu kwa wananchi kwa ujumla.
Jaji Mkuu aliongeza kuwa wananchi wengi wanapoteza haki zao za msingi kwa kutokujua sheria, hivyo kuna umuhimu wa kujua aina za makosa na adhabu zinazoweza kutolewa katika makosa hayo.
“Tangu kuanzishwa kwa sherehe hizi, zimelenga zaidi katika kuhakikisha wananchi wanajua mambo mbalimbali ya kisheria yanayowahusu kwani wengi huwa wanapoteza haki zao za msingi kwa kutokujua sheria, kutokujua sheria haina msamaha katika kosa.” alisema Jaji Mkuu.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni adhabu Mbadala katika kesi za Jinai: Faida zake katika jamii.
Comments