Kifo cha Whitney: hakuna "mkono wa mtu"


Afisa wa uchunguzi mjini Los Angeles, Marekani amesema hakuna dalili za kuwepo na uhalifu katika kifo cha mwimbaji Whitney Houston.

Baada ya kufanya uchunguzi, mtaalam huyo alisema hakuna dalili zozote zinazoonekana kwenye mwili wa Houston na hakuna wasiwasi wa kuwepo na "mkono wa mtu" kwa sasa.

Amesema maafisa bado wanachunguza, lakini hadi wapate matokeo ya uchunguzi mwingine, wataendelea kutazama sababu nyinginezo.

Msanii huyo alikutwa amekufa bafuni katika hoteli moja mjini Los Angeles, siku ya Jumamosi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI