KIWANDA CHA MAGODOLO CHA PAN AFRICA CHATEKETEA KWA MOTO
Kamanda Misime wa kanda ya kipolisi Wilaya ya Temeke akihojiwa na waandishi wa habari mara baada ya kusimamia zoezi la kuzima moto katika kiwanda cha magodolo cha Pan African kilichopo Chang'ombe jijini Dar es salaam, kiwanda hicho kimeteketea kabisa kwa moto uliolipuka kutokana na mlipuko uliotokea kwenye mashine za kunolea visu vya kukata magodolo kiwandani hapo, Kamanda Misime amesema hakuna taarifa ya mtu yeyote kupoteza maisha wala kujeruhiwa katika tukio hilo la moto
Comments