
Katibu Mkuu mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba akipiga mnada suruali wakati wa harambee ya kuchangia mradi wa ujenzi wa kisima cha maji katika Kanisa la Anglikana Parishi ya Mazizini, Ukonga, Dar es Salaam . Zaidi ya sh. milioni 6 zilichangwa ambapo yeye na familia yake walichanga sh. milioni 2.5.

Makamba akiwahamasisha wazee wa kanisa hilo kuchangia kwa moyo wote mradi huo wa kisima

Makamba akiwachangisha waumini wa kanisa hilo

Makamba akihubiri neno la Bwana kabla ya harambee

Wakifurahia muziki wa injili uliokuwa ukiporomoshwa wakati wa harambee hiyo

Moja ya kikundi cha kwaya kikitumbuiza

Msanii wa muziki anayechipukia, Fungo akifanya vitu vyake

Makamba katikati, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kanisa hilo
Comments