Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa shambani kwake Msoga, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. Shamba hilo ni la nyasi za kulishia mifugo kwa njia ya kisasa (zero grazing), akiwa ni mmoja wa wafugaji kijijini hapo. Rais Kikwete, ambaye aghalabu hutumia muda wake wa likizo shambani kwake, pia analima pia mananasi ambayo hustawi vizuri katika wilaya hiyo. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mh Mwantumu Mahiza. PICHA NA IKULU
Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mmoja wa mkazi wa Longido ngombe watano na mbuzi katika sherehe ambayo jumla ya kaya 16 zilikabidhiwa ngombe na mbuzi baadaya kuathirika na janga la kiangazi ambapo baadhi wakazi wa wilaya za Longido,Ngorongoro na Monduli walipoteza mifugo yao yote.Katika zoezi hilo serikali imetoa jumla ya ngombe zaidi ya 25,000 nazaidi ya mbuzi 15,000 ili kuzisaidia familia hizo kuanza tena maisha yao yanayotegemea sana mifugo.Sherehe za makabidhiano hato zilifanyika wilyani Longido, mkoani Arusha leo(picha na Freddy maro).
Comments