TBL YAZINDUA MTAMBO WA KUSAFISHA MAJI TAKA KUWA SALAMA KWA MATUMIZI YA KAWAIDA YA BINADAMU


Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo (kulia), akifunua pazia

kuonesha jiwe la msingi wakati wa uzinduzi wa mtambo wa nne wa

usafishaji maji yaliyotumika kiwandani kuwa maji salama kwa matumizi

ya binadamu katika hafla iliyofanyika katika Kiwanda cha Kampuni ya Bia

Tanzania (TBL) cha Arusha, mwishoni mwa wiki.Anayeshuhudia uzinduzi

wa mtambo huo uliogharimu sh. bilioni 3.6, ni Mkurugenzi Mtendaji wa

TBL, Robin Goetzsche.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo (kulia), akisalimiana na

viongozi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), alipowasili katika hafla ya

uzinduzi wa mtambo wa nne wa usafishaji maji yaliyotumika kiwandani

kuwa maji salama kwa matumizi ya binadamu katika Kiwanda cha

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) cha Arusha, mwishoni mwa wiki.Kutoka

kushoto ni Mkurugenzi wa Ufundi wa TBL, Gavin van Wijk, Meneja wa

Kiwanda TBL Arusha,Bert Grobbelaar na Mkurugenzi Mtendaji wa TBL,

Robin Goetzsche. Wa pili kulia ni Waziri wa viwanda na Biashara ,Dk.

Cyril Chami.


Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo akiwa na viongozi wengine wakitembelea mtambo huo

Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa mtambo huo

Msimamizi wa Mtambo Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) wa kusafisha maji

taka kuwa salama kwa matumizi ya binadamu, Said Lwambo kutoka

Kampuni ya Talbot & Talbot, akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa

Arusha, Magesa Mulongo (wa pili kushoto) na Waziri wa Viwanda na

Biashara, Cyril Chami (wa tatu kushoto) kuhusu usalama wa maji hayo

wakati wa uzinduzi wa mtambo huo uliogharimu sh. bil 3.6 ambao

ulifanyika hivi karibuni katika kiwanda cha TBL Arusha.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.