VODACOM,CCBRT WAZINDUA KAMPENI YA KUCHANGISHA FEDHA SH.BILIONI MOJA ZA UJENZI WA HOSPITALI YA TIBA YA UGONJWA WA FISTULA KWA WANAWAKE
Baadhi ya wanawake wanaosumbuliwa na ugonjwa wa Fistula wanaopata tiba ya bure katika Hospitali ya CCBRT, Msasani, Dar es Salaam, wakiimba kwa furaha wodini kwao, wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni kubwa ya kuchangisha sh. bilioni 1, za kugharamia ujenzi wa Hospitali maalum ya matibabu ya bure kwa wanawake wanaosumbuliwa na ugonjwa wa Fistula nchini. Uzinduzi huo ulifanywa kwa pamoja na Vodacom Tanzania na CCBRT.
Mkurugenziwa Masoko na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Mwamvita Makamba (kushoto), akiungana nao kuimba wimbo wa kuhamasisha wanawake kujitokeza kwenda kutibiwa Fitula katika Hospitali ya CCBRT.
Waandishi wa habari wakiwajibika wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo
Mwamvita Makamba (kushoto), akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo iitwayo Moyo leo katika Hospitali ya CCBRT. Kulia ni Stellah Nzyemba aliyetoa ushuhuda wa kupona ugonjwa wa Fistula baada ya kutibiwa bure katika Hospitali ya CCBRT.
Stellah Nzyemba akitoa ushuhuda wa kupona ugonjwa wa Fistula baada ya kutibiwa bure katika Hospitali ya CCBRT. (Picha zote na Kamanda Mwaikenda wa Blog hii)
Comments