WABUNGE WAKUTANA NA WATAALAM WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2012.

Waziri wa Fedha Mustapha Mkulo akitoa maelezo ya awali kuhusu maendeleo ya kazi za maandalizi ya sensa ya watu na makazi iliyopangwa kufanyika nchini wakati wa semina kati ya wataalam kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu na wajumbe wa kamati ya Maendeleo ya Jamii na Kamati ya Fedha na Uchumi iliyofanyika jana katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma,Hata hivyo waziri Mkulo amefafanua kuwa serikali itahakikisha kuwa sensa hiyo inafanyika kama ilivyopangwa kwa ubora na ufanisi ikilinganisha na sensa zilizopita.
Manaibu waziri wa Fedha Gregory Theu (kushoto) na Pereira Silima(kulia) wakifuatilia masuala mbalimbali kuhusu Sensa ya watu na makazi itakayofanyika mwaka huu wakati semina iliyowahusisha wataalam kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu na wajumbe wa kamati ya Maendeleo ya Jamii na Kamati ya Fedha na Uchumi jana mjini Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya Maendeleo ya Jamii na Kamati ya Fedha na Uchumi wakifuatilia taarifa mbalimbali kuhusu maandalizi ya sense ya watu na makazi itakayofanyika mwaka walipokutana na wataalam kutoka ofisi ya Taifa ya Takwimu jana mjini Dodoma.
Mkurugenzi mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Sensa Dkt. Albina Chuwa akisisitiza jambo kwa wajumbe wa kamati ya Maendeleo ya Jamii na Kamati ya Fedha na Uchumi kuhusu zoezi la sensa ya watu litakalofanyika nchi nzima mwezi Agosti mwaka huu jana mjini Dodoma.

Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

GSM ARIDHIA UJENZI WA UWANJA WA YANGA JANGWANI

WACHEZAJI YANGA WAGOMA KABISA KUFANYA MAZOEZI LEO, LWANDAMINA AIBUKA PEKE YAKE SHAMBA LA BIBI

DKT. MAJULE AMFANYIA MAPOKEZI MAKUBWA BALOZI WA CHINA NCHINI

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

HERSI KWENDA KUSOMA TENA CHUO KIKUU CHA OXFORD UINGEREZA

Wasifu wa Kizza Besigye

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda