EAC YATAKIWA KUIMARISHA VITA DHIDI YA FEDHA HARAMU

Arusha Aprili 30, 2012 (EANA) – Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zinatakiwa kuunganisha nguvu zake kwa pamoja ili kuzuia na kupambana na fedha haramu na ongezeko la ufadhili wa vitendo vya kigaidi katika kanda hiyo.
‘’Nchi za EAC zinaweza kufanikiwa katika kuzuia na kupambana na fedha haramu na ufadhili wa ugaidi kupitia juhudi za pamoja,’’ alisema Waziri wa Usalama wa Burundi, Gabriel Nizigama wakati wa kufungua warsha ya siku nne ya wataalam juu ya fedha haramu na ufadhili wa ugaidi, mjini Bujumbura, Burundi, Juzi.
Kanda hiyo, alisema, inahitaji hatua maalum ya kutambua na kuzuia shughuli za kihalifu kupitia uhifadhi wa kumbukumbu na utambuzi wa wateja na pia utoaji taarifa haraka juu ya shughuli au watu wanaotiliwa mashaka.
Warsha hiyo inayodhuriwa na wataalamu wa kupambana na fedha haramu,kitengo cha usalama wa fedha, mamlaka za mapato, wanasheria, polisi na maafisa usalama imeandaliwa na EAC kwa kushirikiana na serikali ya Australia.
Warsha hiyo ni matokeo ya uamuzi wa mkutano wa nne wa Baraza la Kisekta ya Usalama ambao ulitambua kwamba fedha haramu ni tishio kwa mtangamano wa EAC.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa EAC, anayeshughulikia Shirikisho la Kisiasa, Beatrice Kiraso, alisema kwamba kadiri mtangamano wa EAC unavyozidi kuimarika, ni dhahiri kwamba kuwepo kwa vitendo vya uhalifu hakukwepeki.
‘’Tuna wajibu wa kulinda miundombinu yetu ya fedha na utulivu wa uchumi wetu kama manufaa ya mtangamano wetu yanatakiwa yaonekana,’’ alisisitiza na kuongeza kwamba uhalifu kama usafirishaji wa fedha haramu na ufadhili wa vitendo vya kigaidi lazima vipigwe vita vikali.
Alisema vinginevyo uhalifu huo utaharibu maendeleo ya kiuchumi ndani ya kanda, kuwatisha wawekezaji na kuharibu usalama na utulivu uliopo ndani ya nchi za EAC, alieleza Kiraso katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mtaalamu wa EAC wa Masuala Amani na Usalama, Leonard Onyonyi.
Mwakilishi wa serikali ya Australia, Mike Petty kwa upande wake alisema ushirikiano wa kikanda na kimataifa ni muhimu katika mapambano dhidi ya uhalifu kwa sababu utandawazi siyo tu kwamba unaleta teknolojia na jamii pamoja bali pia wahalifu na uhalifu hatari.
NI

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

MONGELLA AKABIDHIWA ‘MIKOBA’ RASMI YA NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA*

NCHIMBI AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI