Miss Ukonga 2012 walio
chuchumaa wakiwa katika picha ya Pamoja na wartembo wa Miss Tabata 2012 wakati
walipofanya mazoezi ya pamoja jana.
WAREMBO wa vitongoji viwili vya Ukonga na Tabata
jana walifanya mazoezi ya pamoja katika kuleta ushirikiano na kujenga urafiki
baina ya warembo hao katika fani ya urembo.
Warembo wa Tabata waliwatembelea wenzao wa Ukonga
katika kambi yao ya mazoezi iliyopo Ukonga Hill Tech Bar maeneo ya Minazi Mirefu
au maarufu Banana.
Vitongoji vya Ukonga na Tabata warembo wake watakao
shinda wanataraji kukutana katika Kambi ya kanda ya Ilala kabla ya kwenda
kushiriki shindano la taifa la Miss Tanzania 2012.
Wakizungumza jana baadhi ya warembo wa Ukonga
wamesema ushirikiano wao huo na wenzao wa Tabata unawapa uwezo wa kijiamini na
kupata nafasi ya kujifunza kile ambacho wenzao wanakifanya au wamejifunza ikiwa
ni pamoja na utembeaji, uongeaji wa kati wa kujitambulisha na vitu vingine
vingi.
“Tunawashukuiru sana waandaji wetu, maana mbali ya
kuwa tunapata wageni wa aina mbalimbali ambao ni wadau wa urembo lakini leo tupo
na washiriki wenzetu wa tabata ambao tunaimani tutakutana katika shindano la
Ilala”, alisema Amina Sangawe.
Nae Suzanne Deodatus ambaye ni Mshiriki kutoka
Tabata alisema wamepata fursa ya kujifunza mambo kabdhaa na wamefurahi sana
kuwatembelea warembo wa Ukonga na kufnya nao mazoezi ya pamoja.
Mapema Mwezi huu warembo wa Ukonga waliwasindikiza
Miss Tabata 2012 katika show yao kubwa ya Utambulisho iliyofanyika katika Ukumbi
wa Dar West Tabata.
Shindano la Miss Ukonga 2012 linataraji kufanyika
Mei 5, mwaka huu na lile la Tabata linataraji kufanyika mapema mwezi Juni.
Miss Ukonga 2012
wakicheza mziki wa ufunguzi
Baadhi ya waremnbo wa
Tabata wakipita kwa mwendo wa madaha.
Warembo Ukonga wakicheza
ngoma.
Warembo wa Miss Ukonga
2012 wakimwangalia Mshiriki mwenzao kutoka Tabata akipita mbele yao.
Ngoma ya asili nayo imo
na hapa ni kucheza kwenda mbele.
Mwandaaji wa Miss Tabata,
Freddy Ogot (katikati) akiwaeleza jambo waandaaji wa Miss Ukonga
2012.
Comments