Saudi Arabia yafunga ubalozi Misri


Saudi Arabia imemrudisha nyumbani balozi wake nchini Misri na imesema imefunga ofisi zake zote huko, baada ya maandamano ya hasira kulalamika juu ya wakili wa Misri wa kugombea haki za kibinaadamu kukamatwa na wakuu wa Saudi Arabia.
Ubalozi wa Saudi Arabia mjini Cairo
Ahmed El-Gizawy alikamatwa awali mwezi huu alipowasili Saudi Arabia kwa hija.
Wasaudi wanasema alijaribu kuingiza kwa magendo vitu vinavokatazwa, lakini wanaharakati wanasema el-Gizawy alikamatwa kwa sababu aliwahi kupeleka malalamiko juu ya namna wafungwa kutoka Misri wanavotendewa nchini Saudi Arabia.
Mapema juma hili, mamia ya watu waliandamana nje ya ubalozi wa Saudi Arabia mjini Cairo kudai wafungwa hao waachiliwe huru haraka.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

NCHIMBI AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA