Madaktatri na wauguzi wakisukuma ambulance iliyokuwa imembeba, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyakazi, Dk. Steven Ulimboka, alipofikishwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam, baada ya kutekwa na kupigwa na watu wasiojulikana Jumatano Usiku na kutupwa usiku wa Pande, Dar es Salaam.
Dk. Ulimboka amesafishwa leo kwenda India kwa matibabu zaidi baada ya kuonekana hali kuwa mbaya. Gharama za kumtibu akiwa India ni Dola za Kimarekani 40,000.
Ameondoka akiwa chini ya ulinzi mkali wa Madaktari. huku wanaharakati wenye mabango ya kulaani unyama aliofanyiwa Ulimboka wakijitokeza Muhimbili na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salam.
Haikuweza kufahamika mara moja ni nchi gani hasa atapelekwa kutibiwa. Lakini fununu ni kwamba anaweza kupelekwa India au Afrika Kusini.
Dk. Ulimboka amesafishwa leo kwenda India kwa matibabu zaidi baada ya kuonekana hali kuwa mbaya. Gharama za kumtibu akiwa India ni Dola za Kimarekani 40,000.
Ameondoka akiwa chini ya ulinzi mkali wa Madaktari. huku wanaharakati wenye mabango ya kulaani unyama aliofanyiwa Ulimboka wakijitokeza Muhimbili na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salam.
Haikuweza kufahamika mara moja ni nchi gani hasa atapelekwa kutibiwa. Lakini fununu ni kwamba anaweza kupelekwa India au Afrika Kusini.
Comments