POLISI, MSAMA WANASA WATU WANANE WANAOIBA KAZI ZA WASANII NCHINI

MKURUNGEZI wa Kampuni ya Udalali ya Msama,  Alex Msama  akionesha leo jijini Dar es Salaam, CD zenye nyimbo za wasanii walizokamatwa nazo watu 8 baada ya kudurufu kazi hizo za wasanii zenye dhamani ya milioni 25, Watuhumuwa hao wapo katika Kituo cha Polisi Buguruni, Dar es Salaam.
 Alex Msama akichambua cd hizo leo katika Kituo cha Polisi Buguruni, Dar es Salaam.
                                                        Msama akionesha cd hizo
 Msama akizungumza na waandishi wa habari, kuhusu mkakati wa kuendelea kuwakamata watengenezaji na wauzaji wa CD hizo feki.
                                                           Baadhi ya CD zilizokamatwa
  Majina ya watu 8 waliokamatwa wakiuza CD hizo. PICHA ZOTE NA KAMANDA MWAIKENDA


Na Asha Kigundula

MKURUNGENZI wa Kampuni ya Udalali ya Msama,  Alex Msama  akishirikiana na  Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata watu 8 baada ya kudurufu kazi za wasanii zenye thamani ya sh.milioni 25.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Msama alisema wiki iliyopita walianza zoezi la kukamata watu wanaozidurufu kazi za wasanii mbalimbali ambazo wanauza kwa faida yao.

Msama alisema wakiwa maeneo ya Buguruni sheli, walifanikiwa kuzikamata kazi hizo zikiwa zinauzwa kwa bei ya chini.Alisema kuna baadhi ya kazi hata mtaani hazijaanza kutoka lakini wao wanazo na wakiuza kwa shilingi 1000 kila moja.

"Tumekuta kazi mbalimbali kama vile za muziki wa Injili, Movies, nyimbo za bendi muziki wa ndansi na taarab" alisema Msama.Alisema licha ya kukamata CD hizo za kusikiliza na kuonesha ilifanikiwa kukamata mashine moja ya kudurufu.

Msama alisema katika zoezi hilo waliwakamata watu nane wakiwa wanauza kazi hizo.Waliokamatwa ni Halfan Bakari, Hassan Bakari,Hemed Mohamed, Patrick Peter, Hashraf Rajab, Mkoya Peter na Khamis Athuman.

Msama alisema watuhumiwa hao wote wapo katika kituo cha Polisi Buruguruni kwa ajili ya uchunguzi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.