WAKATI Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar
es Salaam likizuia maandamano ya baadhi ya Waislamu yaliyotangazwa kufanyika
Novemba mosi na mbili mwaka (kesho na keshokutwa) kushinikiza kutolewa rumande kwa Katibu wa
Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda, ujumbe mfupi wa
simukuhamasisha maandamano hayo unazidi kusambazwa kwa waisilamu maeneo
mbalimbali.
Raha za Pwani
imefanikiwa kunasa meseji
hiyo ikieleza kwamba siku hiyo shule zote za Kisilamu zitafungwa
ilikutoa
fursa kwa wanafunzi walimu na wazazi wa kisilamu nao kushhiriki kwenda
kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kushindikiza kutolewa kwa sheikh
Ponda ambapo siku ya pili yake (Ijumaa) kufanya
maandamano makubwa jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar
es Salaam, Suleiman Kova, alisema juzi kuwa maandamano hayo ni batili kutokana
na kutopewa baraka na jeshi hilo. Alisema polisi imejipanga kuwashughulikia
wote watakaofanya maandamano katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Aidha, alisema Jeshi la Polisi linamsaka
mtu anayechapisha vipeperushi vya kuchochea maandamano ambayo ni hatari kwa
wananchi. Aliwataka wananchi kuendelea na shughuli za
kiuchumi kutokana na kuimarishwa kwa usalama katika siku hizo ambazo watu hao
wanataka kuandamana kinyume cha sheria.
“Hatutarudi nyuma kwa wale ambao watavunja
sheria na kuvuruga amani ya nchi katika siku hizo mbili,” alisema Kova.
Kova alisema haki itapatikana mahakamani,
hivyo hakuna haja ya kufanya maandamano katika mahakama hiyo ambayo inasikiliza
kesi ya kiongozi huyo
Comments