THE UNITED REPUBLIC
OF TANZANIA
DIRECTORATE OF
PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
THE
STATE HOUSE,
P.O. BOX
9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Kikwete aelekeza viongozi kushughulia njaa
Kilimanjaro
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
ameuelekeza uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro na hasa Wilaya ya Same kufanya
tathmini kamili na ya haraka kujua kiwango cha njaa katika wilaya hiyo ili
kuiwezesha Serikali kutoa chakula cha msaada ama cha bei nafuu kwa wananchi.
Aidha,
Rais Kikwete amesema kuwa Serikali yake itaipatia jawabu la kudumu changamoto
ya maji katika maeneo ya Mkoa wa Kilimanjaro na hasa Wilayani Same.
Rais
Kikwete alitoa agizo la kushughulikia tatizo la njaa jioni ya jana, Jumatatu,
Oktoba 29, 2012, wakati alipoelezwa na wananchi katika maeneo mbali mbali ya
Wilaya ya Same aliposimama mara kwa mara kusalimia wananchi kwenye siku ya pili
ya ziara yake ya siku nne Mkoani Kilimanajaro.
Wananchi
katika maeneo ya Hedaru na Lembeni walimwambia Mheshimiwa Rais Kikwete kuwa
wanakabiliwa na njaa kwa sababu ya ukame ambao umesababisha wasipate chakula
cha kutosha kwa miaka mitatu iliyopita.
Baada
ya kusikiliza malalamiko hayo hasa kuhusu njaa na ukosefu mkubwa wa maji, Rais
Kikwete alisema: “Nimesikia maelezo yenu kuhusu ukosefu wa chakula na njaa. Mkuu wa Mkoa
yupo hapa pamoja na Mkuu wa Wilaya na napenda kuwaagiza wafanye tathmini ya
haraka kuhusu kiwango cha tatizo ili Serikali ichukue hatua ya kumaliza tatizo
hili.”
Aliongeza
Mheshimiwa Rais: “Hakuna wasiwasi. Hakuna mtu ambaye atapoteza maisha yake kwa sababu ya
njaa. Tunacho chakula cha kutosha na Serikali itahakikisha chakula kinapatikana
mara tu tathmini itakapokamilika.”
Aliongeza
Rais Kikwete: “Chakula kitakuwa cha aina mbili. Kwa familia zisizokuwa na uwezo
kabisa chakula kitatolewa bure. Kwa wale wanaojiweza, chakula kitatolewa kwa
wananchi kuchangia fedha kidogo sana kama Sh. 50 tu.”
Rais
Kikwete alisimamishwa mara tisa na wananchi ambao walikuwa na hamu ya kumwona
na kusalimiana naye akiwa njiani kutoka
Mamba Miamba ambako alizindua Kiwanda cha Kusindika Tangawizi kwenda
Mwanga ambako alifungua Hosteli ya Shule ya Wasichana ya Asha Rose Migiro mjini Mwanga.
Imetolewa na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
30
Oktoba, 2012
Comments