Lulu hatimaye aachiwa kwa dhamana na Mahakama Kuu, aangua kilio na mama yake

Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’, akishuka kutoka katika gari lililomleta leo, Mahakama Kuu wakati wa kukamilisha taratibu za kupata dhamana. 

Lulu akiingia Mahakamani huku akisindikizwa na Askari Magereza.
Lulu akiingia mahakamani, huku akitabasamu, akiwa anasindikizwa na askari Magereza.
Lulu akijificha uso, asipigwe picha na waandishi wa habari 'Paparazi' wakati akitoka nje ya Mahakama Kuu, akiwa mamepatiwa dhamana katika ombi lake alililoliwasilisha mahakamani hapo.
Lulu akiingia mahakamani kwenda kukamilisha masharti yake ya dhamana, Dar es Salaam leo.
Lulu akiwa amezungukwa na baadhi ya waandishi wa habari waliotala kufanya naye mahojiano, muda mfupi baada ya kupata dhamana.
Lulu akiangua kilio baada ya kushindwa kuongea na waandishi wa habari waliokusanyika mahakamani hapo.
Lulu akitoka katika lango Kuu la Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam baada ya kupata dhamana.
Lulu akilia wakati akitoka Mahakamani huku nyumba akifuatiwa na mama yake mzazi.
Wasanii nao wallijitokeza mahakamani hapo kumfariji Lulu, kulia ni msanii wa filamu, Muhsin Awadh 'Dk. Cheni'
Lulu akiondoka mahakama hapo.
Wakili anayemtetea Lulu akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya mteja wake kupata dhamana katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo. Lulu amepata dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa serikali waliosaini bondi ya Sh.milioni 20 kila mmoja, kusalimisha hati ya kusafiria, kutotoka nje ya Dar es Salaam  bila ruhusa ya mahakama na kuripoti kwa msajili kila mwezi.  Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba. (Picha zote kwa hisani ya Habari Mseto)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE